JE UMEROGWA? ZIJUE DALILI ZA WAZI


Je, umerogwa? Kuna  watu wengi wanatembea bila kujijua kama wamerogwa. Blog yako hii sasa imeamua kusaidia wananchi kama hawa ili wajijue kama maisha yao yameingiliwa na mkono wa mtu. Kutokana na roho nzuri sana ya mkuu wa blog hii, juzi amewasiliana na mtaalamu kutoka Australia, ili kusaidia  kutoa ushauri hata tiba kwa wale ambao wamejikuta wamelogwa. Kitu cha kwanza ni kujua kama umelogwa au la, zifuatazo ni dalili za wazi kuwa maisha yako yako chini ya mkono wa mtu. Tutakuwa tunaongeza ishara hizi kila zitakapokuwa zinatokea, naomba nimuachie mtaalamu aeleze dalili za kujua umelogwa. Kimsingi ukiwa na moja kati ya yafuatayo tuandikie chini kwenye comment tujue namna ya kukushauri;

1.   Ikiwa umefanya kazi katika kampuni shirika au kwa mtu binafsi miaka kumi bila kupandishwa cheo au kuongezwa mshahara.

2.   Kama kila ukikusanya hela ununue TV unapata janga hela zinatumika

3.   Kama kila ukimuona mwanajeshi unapata hisia za kumzaba kibao

4.   Kama una gari linalokuwa muda mwingi zaidi gereji kuliko barabarani

5.   Kama wewe ni mpenzi damu wa Arsenal

6.   Kama kila ukipigwa picha unatoka hujapendeza

7.   Kama mwanao wa pekee anabwia unga

8.   Panya wamekula jina lako tu kwenye vyeti vyako vya elimu.

9.   Ukijikuta kila ukiwa na ratiba ya kupanda ndege unachelewa

10.  Kila msichana ukimuacha ndio anakuwa mzuri zaidi

11.  Unapokosea na kutumia super glue badala ya matone ya dawa ya macho.

12.  Ukijikuta unaota unapigana na wajumbe

13. Kama kila mwanaume ukimuacha ndio ananunua gari

.Kwa leo mtaalamu ametuacha hapa tukutane tena baada ya siku chache kuongezewa dalili za kurogwa. Tafadhali tuandikie kama unaona kuna kitu kinakuhusu

Categories: Daily Kiswahili Joke

1 reply

Leave a reply to Anonymous Cancel reply